Bunge la kaunti ya Mombasa laweka kikao la kusikiza kuhusu kubadilisha jina la bustani la Mama Ngina Park

Febuari 27, 2020

Bunge la Kaunti ya Mombasa limetangaza Kongamano la hadhara la kujadili kubadilishwa jina kwa eneo la Mombasa linaloitwa Mama Ngina Waterfront Park, ambalo lilifunguliwa mwishoni mwa 2019. Kongamano hilo litafanyika tarehe 4 Machi 2020 saa 9:30 asubuhi katika Ukumbi wa Kijamii wa Tononoka.

Jukwaa hilo limeitishwa kujibu ombi la Okoa Mombasa mnamo Novemba 2019, ambalo liliomba ushiriki wa umma kuhusu suala la kubadilisha jina la mbuga hiyo. Ushiriki huo wa umma unahitajika na Katiba ya Kenya.

Okoa Mombasa inachukulia jina la “Mama Ngina” Waterfront Park kuwa ufutaji na utata wa kipengele muhimu cha historia ya watu wa Mombasa. Tunaamini jina lililochaguliwa linafaa kuashiria kurejelewa kwa urithi wa kihistoria na kitamaduni wa watu wa Mombasa, haswa, na Pwani, kwa jumla.

Okoa Mombasa anawahimiza wananchi wote kuhudhuria. Iwapo huwezi kuhudhuria, unaweza kuwasilisha maoni yaliyoandikwa kwa Bunge kwa barua pepe kwa Countyassemblymombasa@gmail.com au kwa kuwasilisha kwa Ofisi ya Karani, Majengo ya Bunge la Kaunti ya Mombasa SLP 80438-80100.

Maoni yaliyoandikwa lazima yapokewe kabla ya Alhamisi, 5 Machi 2020.

Share This