Mkutano wakufikia wapiga kura: Mei 21 saa 9:30 asubuhi, Majengo Chief’s Hall, Mombasa

Mei 18, 2022
Okoa Mombasa itafanya mkutano wa wazi wa wapiga kura ili kutoa mwelekeo wa Uchaguzi, mkutano utakua tarehe 21 Mei 2022 kuanzia saa 10 asubuhi hadi adhuhuri katika Ukumbi wa Majengo Chief’s mjini Mombasa. Wote mnaalikwa kuhudhuria.

Kongamano hilo linaandaliwa ili kusaidia kukuza na kuunda orodha ya madai za Okoa Mombasa yanayohusiana na matakwa ya wakazi wa Mombasa kwa Uchaguzi wa 2022. Katika wiki zijazo, tutachapisha orodha yetu ya madai na kuwafahamisha wanasiasa na wanaotaka kusaini. Wale wanaotia sahihi watakubali kujumuisha madai katika ilani yao na mpango wa utekelezaji.

Pia tunawaomba wapiga kura kutanguliza upigaji kura kwa wagombea wanaotia saini ahadi hiyo.

Tunatumai kuonana huko.

Tazama kijitabu cha Okoa Mombasa kinachoelezea maeneo ya kuzingatia kwa madai yetu ya Uchaguzi wa 2022.

Angalia kijitabu cha Okoa Mombasa kinachoelezea maeneo ya kuzingatia kwa madai yetu ya uchaguzi wa 2022.

Share This